Close Menu
    Facebook X (Twitter) Instagram
    XXLTZ MEDIA
    Facebook X (Twitter) Instagram
    XXLTZ MEDIA
    Home » Mwanamke ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie ( MAKALA )
    VIDEOS

    Mwanamke ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie ( MAKALA )

    Dj StarBoyBy Dj StarBoyJanuary 18, 2021No Comments4 Mins Read
    Facebook Twitter Telegram WhatsApp
    Download Now

    Mwanamke ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie ( MAKALA )

    1. CHOKOCHOKO
    Wanaume wengi huwa hawapendi chokochoko. Hawapendi mwanamke ambaye yeye kila wakati ni kuanzisha chokochoko ambazo zinazalisha ugomvi. Wanaume wengi hawapendi mabishano.

    Hawapendi ugomvi hivyo mwanamke anapokuwa hodari wa kuleta chokochoko, huepukwa.

    Ni vyema basi mwanamke akachunga kauli. Akawa si mtu wa kuchimbachimba vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Asiwe na kisirani.

    Kinywa chake kitawaliwe na maneno matamu, yatakayomtia moyo mpenzi wake, yatakayomfariji na yatakayomfanya apende kuzungumza naye.

    Mara nyingi mwanaume akiona mke au mpenziwe ni mtu wa kupenda chokochoko, mara nyingi humuepuka. Anajitahidi kadiri ya uwezo wake kukaa naye mbali.

    Ataona ni bora achelewe kurudi nyumbani akakutane na marafiki baa, wapige stori ili muda uende na akirudi nyumbani asiwe na muda wa kuzungumza na mwenzi wake, yeye ni kula na kulala.

    2. KUTORIDHIKA
    Wanaume wengi wanachukia kuwa na wanawake wasioridhika. Baadhi ya wanawake hata uwape nini huwa hawaridhiki.

    Wanawasumbua wapenzi wao kwamba hawawatimizii mahitaji. Mwanaume anajitoa kumpa zawadi mpenzi wake, haridhiki tu.

    Anaanza kuikosoa. Anasema haifanani na yeye, eti si ya hadhi yake. Akipewa fedha anasema hazitoshi. Kila siku ni malalamiko. Hampi nafasi mpenzi wake ya kufurahia uhusiano wao.  Anamfanya kila anapokutana naye awaze atapigwa mzinga.

    Bahati mbaya sasa kila atakachopewa haridhiki. Anatamani kikubwa zaidi. Wanaume wengi siku hizi wanaichukia tabia hiyo. Hawapendi kuwa na mwanamke ambaye haridhiki na kile kidogo walichojaliwa. Wanaume wengi wakiona hivyo huwa wanaanza kumuepuka mwanamke wa ‘sampuli’ hiyo.

    Kwake kunakuwa hakuna jema. Badala ya kumshauri mpenzi wake mbinu za kujikwamua kiuchumi yeye ni lawama tu.

    Kila siku analalamika kwamba wanaume wengine wanawapa wapenzi wao mahitaji muhimu lakini wa kwake hamtimizii.

    Mwanaume akiona kila analofanya kwa mpenzi au mkewe haridhiki, hatoi shukurani ni rahisi kupunguza mapenzi kwa mtu wake. Taratibu anaanza kujitoa na hata kuhamishia mapenzi kwa mtu mwingine ambaye atakuwa anaridhika kwa kidogo anachopewa. Ni muhimu kuridhika.

    3. KULINGANISHA
    Hii nayo ni tabia isiyopendwa na wanaume wengi. Wanaume wanapenda kuishi maisha yao. Wanapenda kuheshimiwa na wapenzi wao.

    Wanapenda kumsikia mwanamke akisema; ‘hakuna mwanaume mwingine wa kufanana na wewe.’

    Mwanaume anapenda kuhakikishiwa kwamba hakuna mwanaume mwingine kama yeye. Yeye ndiye mzuri au bora kuliko wanaume wengine hivyo mwanamke anapoanza kuonesha tabia za kumlimnganisha na mwanaume mwingine linakuwa tatizo kubwa.

    Mwanaume anakasirika. Anaona ni rahisi mwanamke wake kumtamani mtu mwingine baki kuliko yeye.

    Sifa anazozitoa kwa mwanaume mwingine ni nzuri hivyo zinamvutia. Kama zinamvutia siku yoyote anaweza kushawishika kumfuata yule anayemvutia.

    Wanawake wanapaswa kuwa makini katika eneo hilo. Hata kama umeona kuna kitu kizuri kimekuvutia kutoka kwa mwanaume mwingine, kamwe usije kumwambia mwenzi wako. Baki nalo moyoni. Jipe moyo kwamba mwanaume uliyenaye ndiye bora kuliko wanaume wote duniani.

    4. KUWA TEGEMEZI
    Wakati mwingine hata kama huna kitu lakini mwanamke unashauriwa kutojionesha huna kitu.

    Jioneshe kwamba una kitu hata kama huna. Wanaume wa sasa hawapendi kuwa na mwanamke ambaye kila kitu anategemea kutoka kwa mwanaume.

    Hata kama huna kazi lakini ni vyema basi mwanamke akajaribu kufanya biashara ndogondogo ambazo zitampunguzia mwanaume wake makali ya kuombwa fedha kila wakati. Wanaume wanapenda kuwapa wapenzi wao fedha lakini inapozidi kipimo inageuka kuwa kero.

    Yani kuanzia mahitaji ya kila siku, saluni, mavazi, ada ya watoto na mengine mengi mwanamke anamtegemea mwanaume. Yeye hataki kujishughulisha hata kidogo. Anataka aletewe, kazi yake kubwa ni kulea familia nyumbani.

    Mwanaume akigundua mwanamke ni tegemezi mkiwa katika hatua za mwanzoni, ni rahisi kumkimbia mwanamke na kwenda kwa mwanamke ambaye angalau atakuwa hamtegemei kwa kila kitu.

    Mwanamke anayejiongeza hata kwa kutoa wazo la kuanzishiwa biashara ambayo itamfanya asiwe tegemezi.

    5. KUTOKUA MUELEWA
    Mwanaume anapenda mwanamke muelewa. Hapendi mwanamke mbishi. Anatamani kuwa na mwanamke ambaye akimueleza kitu, anajiongeza na kufanya zaidi ya pale mwanaume alipofikiria.

    Mwanaume anapenda mwanamke atakayeanzisha wazo la kimaendeleo na kumshirikisha mpenzi wake ili walifanye.

    Wanaume wanapenda wanawake wanaowaelewa. Kama mwanamke anakuwa si wa kumuelewa mpenzi wake, kumsaidia basi mara nyingi mwanaume humkimbia.

    6. KUJITAPA KWA KUWA NACHO
    Hakuna mwanaume anayependa kutawaliwa. Wanawake wenye fedha mara nyingi wanakuwa na tabia ya kutaka kuwatawala wanaume.

    Anataka mwanaume afanye kile ambacho yeye anataka. Fedha zinamvimbisha kichwa na kuona kwamba anaweza kuwa na mamlaka ya kumuamrisha mumewe.

    Anatumia fedha zake kama fimbo ya kumchapia mpenzi wake. Ni vigumu sana wanaume kumvumilia mwanamke wa aina hiyo, mara nyingi wanajiepusha naye.

    Kwa kutumia fedha zake anaweza kupata mwanaume mwingine lakini pia watashindwana katika suala la kumtawala.

    7. KUWA BIZE SANA
    Wanaume wengi hawapendi mwanamke tegemezi lakini pia wanaume haohao wanachukia mwanamke akiwa bize sana na kazi zake.

    Mwanaume hapendi kuona mwenzi wake anakuwa bize na kazi au biashara zake kiasi ambacho kitamfanya hata akose muda na mwenzi wake.

    Unachotakiwa kufanya hapo mwanamke ni kujigawa. Hakikisha unakuwa bize na kazi lakini si ya kupitiliza maana itamfanya mwanaume akose muda wa kuwa na wewe pale anapokuhitaji, badala yake anaweza kwenda kwa mwanamke mwingine ambaye hayupo bize

    Download Now
    Hadithi
    Share. Facebook Twitter Pinterest Telegram WhatsApp Copy Link
    Dj StarBoy
    • Website

    Related Posts

    VIDEO | D Voice – Mbwa

    April 24, 2025

    VIDEO | Kmc Arusha Cathedral – Israeli Yatetema

    April 19, 2025

    VIDEO | Hisili Music Ft. Wamwiduka Band – Twende Pamoja

    April 19, 2025
    Leave A Reply Cancel Reply

    LATEST POST
    AUDIO

    AUDIO Dami – Lock Down Download Mp3

    By Dj StarBoyMay 3, 20250

    AUDIO Dami – Lock Down Download Mp3 https://cldup.com/igusma4jZx.mp3?download=Dami%20-%20Lock%20Down.mp3 Download Mp3

    AUDIO Mr Blue – Aisha Download Mp3

    May 1, 2025

    AUDIO Yee Fant Ft Chiboo – Madamu Mp3 Download

    May 1, 2025

    AUDIO Yampano – Inzobe Mp3 Download

    May 1, 2025

    AUDIO Jay Melody – Jirani Mp3 Download

    May 1, 2025

    AUDIO Meja Kunta – Siyawezi Mp3 Download

    May 1, 2025

    AUDIO | Appy Ft. Kontawa – Mdogo Mdogo | Download Mp3

    April 24, 2025

    AUDIO | Chalii Boy – Bora Niveshe | Download Mp3

    April 24, 2025

    AUDIO | Dogo Mallo Og – Kila mtu Na Maisha Yake | Download Mp3

    April 24, 2025

    VIDEO | D Voice – Mbwa

    April 24, 2025
    LATEST POST

    AUDIO Dami – Lock Down Download Mp3

    May 3, 2025

    AUDIO Mr Blue – Aisha Download Mp3

    May 1, 2025

    AUDIO Yee Fant Ft Chiboo – Madamu Mp3 Download

    May 1, 2025

    AUDIO Yampano – Inzobe Mp3 Download

    May 1, 2025
    TRENDING POST

    AUDIO | Zuchu – Afande | Download Mp3

    April 21, 2025

    AUDIO | Harmonize – Yeye | Download Mp3

    April 20, 2025

    AUDIO | Jay Melody – Mtoto | Download Mp3

    April 20, 2025

    AUDIO | Diamond Platnumz – Kuna | Download Mp3

    April 17, 2025
    Live Mganga Akitoa Vitu Vya Ajabu Tanga
    Video Player
    https://www.youtube.com/watch?v=Y8AVdzd7iO4&t=7s
    00:00
    00:00
    03:03
    Use Up/Down Arrow keys to increase or decrease volume.
    Facebook X (Twitter) Instagram Pinterest
    © 2025 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.