Close Menu
NYIMBO MPYA 2025NYIMBO MPYA 2025
    Facebook X (Twitter) Instagram
    NYIMBO MPYA 2025NYIMBO MPYA 2025
    • MUSIC
    • ALBUM / EP
    • Dj Mix
    • Gospel
    • ON TRENDING
    • Contact Us
    • Privacy Policy
    Facebook X (Twitter) Instagram
    NYIMBO MPYA 2025NYIMBO MPYA 2025
    Home » Mwanamke ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie ( MAKALA )
    Uncategorized

    Mwanamke ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie ( MAKALA )

    Dj StarBoyBy Dj StarBoyJanuary 18, 2021No Comments4 Mins Read
    Facebook Twitter Pinterest Telegram WhatsApp

    Mwanamke ukiwa na tabia hizi 7, lazima mwanaume akukimbie ( MAKALA )

    1. CHOKOCHOKO
    Wanaume wengi huwa hawapendi chokochoko. Hawapendi mwanamke ambaye yeye kila wakati ni kuanzisha chokochoko ambazo zinazalisha ugomvi. Wanaume wengi hawapendi mabishano.

    Hawapendi ugomvi hivyo mwanamke anapokuwa hodari wa kuleta chokochoko, huepukwa.

    Free stream and download music Nyimbo Mpya 2025 including the best new songs, albums and curated playlists on XXLTZ MEDIA and play, offline data free

    PAKUA NYIMBO MPYA 2025 HAPA

    Ni vyema basi mwanamke akachunga kauli. Akawa si mtu wa kuchimbachimba vitu ambavyo havina kichwa wala miguu. Asiwe na kisirani.

    Kinywa chake kitawaliwe na maneno matamu, yatakayomtia moyo mpenzi wake, yatakayomfariji na yatakayomfanya apende kuzungumza naye.

    Mara nyingi mwanaume akiona mke au mpenziwe ni mtu wa kupenda chokochoko, mara nyingi humuepuka. Anajitahidi kadiri ya uwezo wake kukaa naye mbali.

    Ataona ni bora achelewe kurudi nyumbani akakutane na marafiki baa, wapige stori ili muda uende na akirudi nyumbani asiwe na muda wa kuzungumza na mwenzi wake, yeye ni kula na kulala.

    2. KUTORIDHIKA
    Wanaume wengi wanachukia kuwa na wanawake wasioridhika. Baadhi ya wanawake hata uwape nini huwa hawaridhiki.

    Wanawasumbua wapenzi wao kwamba hawawatimizii mahitaji. Mwanaume anajitoa kumpa zawadi mpenzi wake, haridhiki tu.

    Anaanza kuikosoa. Anasema haifanani na yeye, eti si ya hadhi yake. Akipewa fedha anasema hazitoshi. Kila siku ni malalamiko. Hampi nafasi mpenzi wake ya kufurahia uhusiano wao.  Anamfanya kila anapokutana naye awaze atapigwa mzinga.

    Bahati mbaya sasa kila atakachopewa haridhiki. Anatamani kikubwa zaidi. Wanaume wengi siku hizi wanaichukia tabia hiyo. Hawapendi kuwa na mwanamke ambaye haridhiki na kile kidogo walichojaliwa. Wanaume wengi wakiona hivyo huwa wanaanza kumuepuka mwanamke wa ‘sampuli’ hiyo.

    Kwake kunakuwa hakuna jema. Badala ya kumshauri mpenzi wake mbinu za kujikwamua kiuchumi yeye ni lawama tu.

    Kila siku analalamika kwamba wanaume wengine wanawapa wapenzi wao mahitaji muhimu lakini wa kwake hamtimizii.

    Mwanaume akiona kila analofanya kwa mpenzi au mkewe haridhiki, hatoi shukurani ni rahisi kupunguza mapenzi kwa mtu wake. Taratibu anaanza kujitoa na hata kuhamishia mapenzi kwa mtu mwingine ambaye atakuwa anaridhika kwa kidogo anachopewa. Ni muhimu kuridhika.

    3. KULINGANISHA
    Hii nayo ni tabia isiyopendwa na wanaume wengi. Wanaume wanapenda kuishi maisha yao. Wanapenda kuheshimiwa na wapenzi wao.

    Wanapenda kumsikia mwanamke akisema; ‘hakuna mwanaume mwingine wa kufanana na wewe.’

    Mwanaume anapenda kuhakikishiwa kwamba hakuna mwanaume mwingine kama yeye. Yeye ndiye mzuri au bora kuliko wanaume wengine hivyo mwanamke anapoanza kuonesha tabia za kumlimnganisha na mwanaume mwingine linakuwa tatizo kubwa.

    Mwanaume anakasirika. Anaona ni rahisi mwanamke wake kumtamani mtu mwingine baki kuliko yeye.

    Sifa anazozitoa kwa mwanaume mwingine ni nzuri hivyo zinamvutia. Kama zinamvutia siku yoyote anaweza kushawishika kumfuata yule anayemvutia.

    Wanawake wanapaswa kuwa makini katika eneo hilo. Hata kama umeona kuna kitu kizuri kimekuvutia kutoka kwa mwanaume mwingine, kamwe usije kumwambia mwenzi wako. Baki nalo moyoni. Jipe moyo kwamba mwanaume uliyenaye ndiye bora kuliko wanaume wote duniani.

    4. KUWA TEGEMEZI
    Wakati mwingine hata kama huna kitu lakini mwanamke unashauriwa kutojionesha huna kitu.

    Jioneshe kwamba una kitu hata kama huna. Wanaume wa sasa hawapendi kuwa na mwanamke ambaye kila kitu anategemea kutoka kwa mwanaume.

    Hata kama huna kazi lakini ni vyema basi mwanamke akajaribu kufanya biashara ndogondogo ambazo zitampunguzia mwanaume wake makali ya kuombwa fedha kila wakati. Wanaume wanapenda kuwapa wapenzi wao fedha lakini inapozidi kipimo inageuka kuwa kero.

    Yani kuanzia mahitaji ya kila siku, saluni, mavazi, ada ya watoto na mengine mengi mwanamke anamtegemea mwanaume. Yeye hataki kujishughulisha hata kidogo. Anataka aletewe, kazi yake kubwa ni kulea familia nyumbani.

    Mwanaume akigundua mwanamke ni tegemezi mkiwa katika hatua za mwanzoni, ni rahisi kumkimbia mwanamke na kwenda kwa mwanamke ambaye angalau atakuwa hamtegemei kwa kila kitu.

    Mwanamke anayejiongeza hata kwa kutoa wazo la kuanzishiwa biashara ambayo itamfanya asiwe tegemezi.

    5. KUTOKUA MUELEWA
    Mwanaume anapenda mwanamke muelewa. Hapendi mwanamke mbishi. Anatamani kuwa na mwanamke ambaye akimueleza kitu, anajiongeza na kufanya zaidi ya pale mwanaume alipofikiria.

    Mwanaume anapenda mwanamke atakayeanzisha wazo la kimaendeleo na kumshirikisha mpenzi wake ili walifanye.

    Wanaume wanapenda wanawake wanaowaelewa. Kama mwanamke anakuwa si wa kumuelewa mpenzi wake, kumsaidia basi mara nyingi mwanaume humkimbia.

    6. KUJITAPA KWA KUWA NACHO
    Hakuna mwanaume anayependa kutawaliwa. Wanawake wenye fedha mara nyingi wanakuwa na tabia ya kutaka kuwatawala wanaume.

    Anataka mwanaume afanye kile ambacho yeye anataka. Fedha zinamvimbisha kichwa na kuona kwamba anaweza kuwa na mamlaka ya kumuamrisha mumewe.

    Anatumia fedha zake kama fimbo ya kumchapia mpenzi wake. Ni vigumu sana wanaume kumvumilia mwanamke wa aina hiyo, mara nyingi wanajiepusha naye.

    Kwa kutumia fedha zake anaweza kupata mwanaume mwingine lakini pia watashindwana katika suala la kumtawala.

    7. KUWA BIZE SANA
    Wanaume wengi hawapendi mwanamke tegemezi lakini pia wanaume haohao wanachukia mwanamke akiwa bize sana na kazi zake.

    Mwanaume hapendi kuona mwenzi wake anakuwa bize na kazi au biashara zake kiasi ambacho kitamfanya hata akose muda na mwenzi wake.

    Unachotakiwa kufanya hapo mwanamke ni kujigawa. Hakikisha unakuwa bize na kazi lakini si ya kupitiliza maana itamfanya mwanaume akose muda wa kuwa na wewe pale anapokuhitaji, badala yake anaweza kwenda kwa mwanamke mwingine ambaye hayupo bize

    Hadithi
    Share. Facebook Twitter Pinterest Telegram WhatsApp Copy Link
    Dj StarBoy
    • Website

    Related Posts

    Hello world!

    June 23, 2025

    Hello world!

    June 18, 2025
    Add A Comment
    Leave A Reply Cancel Reply

    TRENDING POST
    AUDIO MPYA

    AUDIO | D Voice Ft Mzee wa Bwax – Ganda | Download Mp3

    By Dj StarBoyJuly 21, 20250

    AUDIO | D Voice Ft Mzee wa Bwax – Ganda | Download Mp3 Listen to…

    AUDIO | Marioo – MVUA | Download Mp3

    July 21, 2025

    AUDIO | Harmonize – Coming Home | Download Mp3

    July 13, 2025

    AUDIO | Meja Kunta Ft Harmonize – Jina | Download Mp3

    July 9, 2025

    AUDIO | Alikiba – Ubuyu | Download Mp3

    July 4, 2025

    AUDIO | G Nako Ft Zuchu – Hapo | Download Mp3

    July 4, 2025

    Diamond Platnumz – Ft. Xman Rsa, Lintonto & Masterpiece_Yvk – Down

    June 27, 2025

    Harmonize Ft Rudeboy – Best Couple

    June 27, 2025

    Diamond Platnumz Ft. Bien – Katam | Download Mp3

    June 10, 2025

    AUDIO | Yammi – Raha | Download Mp3

    June 5, 2025
    Stay In Updates
    • Facebook
    • Instagram
    • YouTube
    • TikTok
    • Telegram
    • WhatsApp
    Don't Miss
    AUDIO MPYA

    AUDIO | Nandy Ft Marioo – Tonge Nyama | Download Mp3

    By Dj StarBoyJuly 24, 20250

    AUDIO | Nandy Ft Marioo – Tonge Nyama | Download Mp3 Listen to the Latest…

    AUDIO | Nandy Ft Marioo – Bia Nyama | Download Mp3

    July 23, 2025

    AUDIO | Dj Robby Fighter Ft MC Shallo – IKO POA | Download Mp3

    July 23, 2025

    AUDIO | Mwakatobe – Uongo | Download Mp3

    July 23, 2025

    AUDIO | Misso Misondo – Ashante Shana | Download Mp3

    July 23, 2025

    AUDIO | Easyman Ft. Isha Mashauzi – Siyawezi | Download Mp3

    July 23, 2025

    AUDIO | Reyd TZ – Kopa | Download Mp3

    July 23, 2025

    AUDIO | Raphael Mgina – Pokea Zawadi | Download Mp3

    July 22, 2025

    AUDIO | Shebby Love – Forever | Download Mp3

    July 22, 2025

    AUDIO | J SILIVA – BOLA POMBE | Download Mp3

    July 22, 2025
    © 2025 ThemeSphere. Designed by ThemeSphere.
    • HOME
    • MUSIC
    • ON TRENDING MUSIC
    • About Us
    • Contact Us
    • Terms of Service
    • Privacy Policy

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.