Browse

Categories

Company

SIMULIZI >UJUMBE KWA WAKE ZANGU

Posted On: March 30, 2017 By NYIMBO MPYA 2024
Stream and Download Nyimbo Mpya 2024 Bongo Fleva Mpya 2024 latest new Songs released 2024 from your favorite Artists and enjoy Mp3 Music Audio and HD New Song Videos of different Styles such as Bongo flava, Hip Hop, Afrobeats, Kwaito, House, Amapiano, Gospel, Zouk/Rhumba & More.

Download Nyimbo Mpya

PLAY
SHARE
   29

”Katika dunia yetu ya leo malezi ni suala ambalo halipatilizwi sana, wazazi wamekuwa wapuuzaji hivyo kufanya vijana wa kiume kutotambua maana ya uanaume wao na vijana wa kike
kutoiona thamani yao, kama muandishi nimeona haja yakukumbushia suala la malezi kwa mtindo huu…ifuatayo ni barua kwa wakwe zangu”

Na
BIN ZONGO

Bado sijaoa lakini naamini ipo kaya moja duniani hapa anaishi mwanamke nitakayemuoa na pengine analelewa na wazazi wake Ujumbe huu nataka ufike kwao…
Ujumbe huu uwafikie wakwe zangu na najua mtastaajabu sababu bado binti yenu hamjamuozoesha wala pia barua ya posa hamjapokea.
me naamini ninyi ni wakwe zangu na sitasita kuwaita hivi sababu wahenga walisema NDOA HUFUNGWA MBINGUNI.
mimi na binti yenu tayari tumeshafunga ndoa mbinguni hata kabla nafsi zetu hazijaletwa hapa duniani.
nimewahi kuwaletea waraka huu wa barua ili kuwajulisha mengi ninayoyataka muyafanye kabla sijakutana na binti yenu.
naandika ujumbe huu nikiwa sina hata dalili yakuoa na wala sijui binti yenu yupoje lakini sababu naamini itafika wakati nitamuoa basi naombeni sana mumtunze vema.
mie bado ningali shuleni, nina uhakika hata yeye kwa sasa anasoma, hakikisheni mnamuhimiza basi asome kwa bidii maana dunia hii haimthamini mtu mjinga kabisa.
mwambieni apambane, aje kuwa mwanamke wa shoka mwenye kujiamini na aweze kujenga hoja zenye mashiko kwa lolote litakalomkabili mbele yake.
nataka akiwa mwanasiasa awe mwanasiasa ambaye hajawahi kuzaliwa duniani hapa au akisema awe mjasiriamali basi asimame imara kushinda wajasiriamali wanaotazamwa hii leo, laa kama jaala yake ni sanaa basi aje aifanye sanaa kwa mtindo utakaofanya hata ardhi itikisike kwa utashi wake.
muandaeni aje kuwa nuru kwenu na kwa familia yake atakayoijenga namimi.
nawaomba wakwe zangu muyatazame haya wayafanyayo mabinti wakileo kwa jicho la laana na msichoke kumlaani shetani asimsogelee binti yenu akapata kumshawishi ayaige.
zamani stara ilikuwa ngao yakumtambulisha binti mwema lkn siku hizi wadada wanapuyanga wakiwa nusu utupu, mkemeeni mke wangu kabla sijajuana nae,mwambieni mumewe sifurahii urembo wakujidhalilisha.
mwambieni ajue mie ni mfuasi wa haiba za kike zilizotiwa nakshi za nidhamu,utu wema na uchamungu mwambieni kamwe sitadumu nae kwenye ndoa kama akiwa mwingi wakuiga yaso na mana.
mwambieni mtoto wenu ajue mimi ndie yule wa ubavu wake niliyefunga nae ndoa mbinguni, hata mimi siamini hili wakati mwengine lkn ukweli ndio huo baada yakufunga ndoa yetu mbinguni tumeletwa duniani, kupoteana kwetu haimaanishi kuwa hatutaonana mwambieni ajue tutaonana na ndoa ile ya mbinguni tutairudia tena duniani.
mkumbusheni hili na mumsisitize awe mwingi wa subira maana ni wengi sana watakuja kwake na kwenu wakidai kuwa ndio wahalali.
toeni muda msikurupuke wazee wangu mkahadaika na posa na shilingi mbili tatu kisha mkamuuza mke wangu kwa waroho wa miili ya warembo.
tambueni mimi nipo na wakati wangu ukifika nitajitokeza mbele yenu na kila kitu kitaenda barabara sababu ndoa yetu tayari ilishapita mbinguni kwa MUNGU.
sio kila mtu anafaa kuwa rafiki wa binti yenu nawaomba sana msiruhusu mashosti wakamuharibu mana nitawalaumu ninyi kwa uhuru wenu mliompa.
samahani baba angu mkwe, naomba niongee nawe! kuchapa mtoto sio kumfunza naomba tumia busara kuongea nae kwa utaratibu hicho kipigo unachompa kinamtia usugu utanifanya nioe gendaeka lisiloogopa hata sauti yangu ikimfokea.
muelekeze kwa upole mwambie unavyopenda awe, usimvunje moyo katika ndoto zake na pia mkataze asipende vya bure, vijana wengi wanaweza kutumia nafasi hiyo kumgeuza chakula chao.
Mpeni sifa zangu, mwambieni mimi nipo naandaliwa vema na wazazi wangu ili nije kuwa mume bora kwake,
Mwambieni mama yangu kila siku ananisisitiza sana kuijua thamani ya mwanamke na baba akizungumza nami ananisisitiza kupambana ili nije kuimudu familia yangu, kumtunza mke wangu na kutokimbia majukumu yangu.
mwambieni binti yenu ajue mimi sihangaiki na wanawake sababu najua yeye yupo na itakuwa vema naye akifanya hivyo.
mwambieni athari zakuruka ruka kabla ya ndoa yetu atapata mimba asizozitarajia, na pengine atawaza dhambi yakutoa jambo ambalo litafanya aniharibie mtoto wangu wakwanza aliyepangwa azae na mimi.
haya mimba atatoa je maradhi yasiyo na tiba, mwambieni tu avumilie mengi matamu atakula na mie maana akifa kabla yamie kumuoa ni dhahiri atakuwa amemkosea MUNGU kwa kukiuka mipango yake na pia ataniachia kovu la maisha kwa mie kuoa asiye wa halali yangu.
naomba ajue hili ndoa nyingi hivi sasa zinavunjika kwa sababu hii, hakika nina mengi sana yakuwaomba wakwe zangu muhakikishe mnayafanya kwa binti yenu ili msije kupata dhambi kuniozesha mke wa mtaa mzima mnaoishi.
mchunguzeni mapema ili mjue kama angali bado ana usichana mwambieni wasahihi kuuona ni mie anisubirie maana tangu nijue ipo siku nitkuwa mume wa mtu sitaki hata binti aniite “baby” nazichunga sana nyendo zangu.
mama mkwe naomba uzingatie, muite binti yako umwambie ipo siku atakuwa mke wa mtu, mpe siri zote za kwanini wewe umedumu kwenye ndoa na mumeo kwa miaka mingi.
mwambie madini yako yanayomfanya mzee asing’oke kwako, mueleze namna ambavyo unalimudu jiko na mtambie kuwa wewe ni mwanamke imara lakini haukuwahi kutambulishwa hata siku moja na mawigi ya rangi rangi au nguo za kiuwenda wazimu mueleze ajue kuwa ulimi wako ndio ngao kwa mumeo.
kuulinda kwako ndio mana mmedumu mpka leo.
nawaachia jukumu wakwe zangu kunilindia mke wangu mpka nitakapokuja mwenyewe kuhalalisha ndoa yangu.
mwambieni nilipo namuombea ili aje kuwa faraja nanuru kwangu na kwa familia yangu.

More from SIMULIZI >UJUMBE

SIMULIZI >UJUMBE KWA WAKE ZANGU   
Posted On:  March 30, 2017

Featured Artists  View All