Browse

Categories

Company

MTU NA TUWE; SEHEMU YA KWANZA

Posted On: March 30, 2017 By NYIMBO MPYA 2024
Stream and Download Nyimbo Mpya 2024 Bongo Fleva Mpya 2024 latest new Songs released 2024 from your favorite Artists and enjoy Mp3 Music Audio and HD New Song Videos of different Styles such as Bongo flava, Hip Hop, Afrobeats, Kwaito, House, Amapiano, Gospel, Zouk/Rhumba & More.

Download Nyimbo Mpya

PLAY
SHARE
   36

IMG-20170327-WA0003“Zawadi nzuri ambayo nipo nayo na nitakuwa nayo daima ni talanta ya uandishi niliyojaaliwa na Mungu, nalazimika kukuzawadia simulizi hii nzuri ya Mapenzi katika msimu huu wa Mahusiano mema kwa wapendanao, msimu wa valentine day, NI KISA CHAKUBUNI AMBACHO NIMEJITAHIDI KUKIMEGA KATIKA SIMULIZI YANGU NZIMA IITWAYO MTU NA MTUWE, NIMEWEZA KUMEGA BAADHI YA VIPANDE NIKAPATA SEHEMU YA KWANZA NA YAPILI…..SONGA NAYO”

NA. OMAR A. ZONGO

Mie na valentine wangu tulikuwa nayo desturi yakutazama habari za ulimwengu kupitia Shirika la utangazaji la CNN.
hii ilikuwa ni asubuhi mishale ya saa ni saa kumi na mbili.
miongoni mwa habari zilizonishangaza ni ile iliyosema kuwa eti Siku ya wapendanao kwa mwaka huu itaadhimishwa kwa maajabu makuu.
Habari hii ilieleza kuwa kutokana na dhulma na kuibiana wapenzi
mwaka huu mioyo ya watu imeamua kufunguka na kueleza kwa vitendo ni yupi anapendwa kwa dhati.
habari ile ilisema kuwa uongo wote katika mapenzi utakoma siku ya tarehe 14 mwezi febr.
Mpenzi wangu alinitazama huku uso wake ukionekana wazi una mastaajabio na maswali mengi kuhusu taarifa ile.
“inawezekana vipi???” akajikuta akihoji hivi.
sorry sijawatajia jina mpenzi wangu huyu anaitwa Jamila.
miongoni mwa wanawake warembo waliofanikiwa kuuteka nyara moyo wangu, mpole na mjuzi wa mambo hasa awapo kwenye ule uwanja wafundi seremala.
nilikosa chakumjibu Jamila wangu kichwani mwenyewe nikabaki nikiitafakari taarifa ile, yaani kama ingekuwa imetangazwa kwenye chombo cha habari cha kawaida ningehisi ni mbinu yakuteka tu wasikilizaji katika siku hiyo ya wapendanao.
nilijaribu kufuatilia media nyengine hakukuwa na taarifa ile mpaka nikahisi labda nimejichanganya mwenyewe kutokana na CNN wanazungunza kiingereza huenda wakawa wameniacha, Lugha Gongana.
tulijadili kidogo na hubby mwisho tukaangukia kwenye utani.
“hivi kama ikiwa nikweli itakuaje swthert maana kila mmoja ataangukia kwa ampendae mnh hivi wewe utabaki namimi kweli???” nilijkuta nahoji kuhusu tafakuri yangu ndogo iliyokuwa ikikatiza kichwani mwangu.
jamila alicheka kisha akanijibu “ah niende wapi mie nishazama kwako” alijibu hivi Jamila, jibu ambalo lilinifariji sana.
asubuhi ile tukaagana vizuri na Jamila mpenzi wangu nikaelekea kazini, wakati niko kwenye gari langu naendesha huku nasikiza redio mojawapo maarufu nchini tanzania ghafla nikaanza kuwasikia watangazaji wakiulizana kuhusu taarifa ile niliyoisikia asubuhi
umakini wakusikiliza ukaongezeka, hata watangazaji wenyewe walikuwa hawaamini kuhusu taarifa ile huku wengi wakihoji itawezekana vipi.
kwa mujibu wa CNN walieleza kuwa ule ni utafiti uliofanywa na wanasaikolojia wa HUBA kutoka katika ulimwengu wa mapenzi ambao haujulikani upo upande gani mwa dunia hii.
huwezi amini
mitandaoni mada ikawa ndio hiyo, jumbe fupi za kuchekesha ziliundwa fasta watu wakitumiana.
mojawapo ni hii
‘pale valentine hii unapojikuta unamuacha uliye nae nakuelekea mirembe maana umpendae yupo huko’
meseji za namna hii zilisambaa kote huku kila mmoja akielekezea hisia zake kuhusu suala lile.
wengi walikuwa kama mimi ilikuwa ni ngumu kuamini kama inawezekana ikawa hivyo.
ilikuwa ni baada ya siku ile ndio siku ya wapendanao ifike wengi walisema haiwezekani huku wakiisubiri kwa hamu ile siku ifike.
nakumbuka siku ile nilifanya kazi mpaka saa mbili usiku nikarejea nyumbani.
wakati naendesha gari mawazo yangu yote yalikuwa kwa Jamila Mpenzi wangu, niliwaza nakuwazua nikitu gani nifanye vilentine hii kumfurahusha hubby wangu.
kutokana na foleni barabarani siku ile nilifika nyumbani saa nne kasoro usiku, kwakweli nilichokikuta siikutaka kuamini.
Jamila alikuwa amepoteza kabisa furaha yake ya siku zote, nilijikuta nambembeleza sana aseme tatizo.
Baadae akawa tayari kunieleza, Loh! nilijuta kumbembeleza.
ni kitambo sana hajamgusia mpenzi wake wa kwanza aliyeitwa Edi, jamaa alimuumizaga sana Jamila enzi wapo wote.
mpaka nampata mimi Jamila bado alikuwa anampenda sana Edi, alikuwa hawezi kupitisha muda flani bila kumtaja mshkaji.
ilikuwa inaniumiza sana hali ile lakini sikuchoka sababu nilikuwa nampenda sana Jamila, nashukuru baada ya muda akanizoea na tukaishi wote kwa furaha na mipango ya harusi yetu ilikuwa inakaribia.
nilishangaa sana kauli zake za siku ile alidiriki kusema kuwa anajilazimisha tu kunipenda lkn moyo wake wote bado upo kwa Edi.
Ulikuwa ni ukweli mithili ya msumari wa moto kwenye mtima wangu.
usoni mwake Jamila alionekana akimaanisha anachosema.
wakati nimepigwa na bumbuwazi ghafla mlangoni kuna mtu alikuwa akibisha hodi.
mimi nilienda kufungua, duh! alikuwa ni Victoria, mpenzi wangu nilieachana nae huyu binti alikuwa ananipenda sana! niliachana nae tu sababu moyo wangu ulizama zaidi kwa Jamila.
Victoria alikuwa ametota machozi! aliniambia amefuata penzi lake.
HABARI ILE YA ASUBUHI ILIKUWA INA UKWELI MBONA MAMBO HAYA SIYAELEWI! NILITAZAMA SAA ZILIBAKI DAKIKA CHACHE TU IFIKE SAA SITA SIKU IBADILIKE IWE SIKU YA VALENTINE DAY!
sorry sijawatajia jina langu Mimi Naitwa Dulla
balaa hili linamuendelezo wake sehemu ya pili USIKOSE KUFUATILIA.
blog hii kwa simulizi nzuri za kila aina

    More from MTU NA

Featured Artists  View All